Go Back   Mashada Forums » Society & Culture » General Discussion
Connect with Facebook

Notices

Reply
 
LinkBack Thread Tools Display Modes
  #21 (permalink)  
Old 4th July 2008, 04:47 PM
Senior Member
 
Join Date: May 2008
Location: Nyumbani kwa mama yangu
Posts: 4,384   (View Stats)
Alja is on a distinguished road
Not Ranked  0 score     
Default    Show Printable Version  Print   Email this Page  Email  

Quote:
Originally Posted by sdolphin View Post
Akii this is so sad (for me) you guys might as well be speaking double dutch backwards. Anti nyita
Tembea na yesu, Amen, Tembea na yesu Amen, halleluya Amen - that sounds Dutch

Tulia dada, ama ni kaka? Wenye walewa lugha mfuti na wale watafsiri halisi watakusaidia.
Reply With Quote
  #22 (permalink)  
Old 5th July 2008, 02:04 AM
Senior Member
 
Join Date: Oct 2007
Posts: 1,212   (View Stats)
Titchaz is on a distinguished road
Not Ranked  0 score     
Default Swala La Mihadarati

Jay-R kwanza kabisa heshima yako mbele,
kabla sijhaendelea nadhani unaongealea mitaa ya old town
na vitongoji f'lani Mombasa.Kumbuka kwa sasa hii ishu imetanda
kote kote na imekua kama kansa!

Kisha nikashamaliza salamu inabidi nirudie mada husika kwa
mtazamo wa kiini hasa cha mihadarati yenyewe kuwepo.
Asikwambie mtu kua masikini nd'o chanzo bali ni hawa viongozi
wetu vizabizabina ambao badala ya kufanya mambo yanayokuza
nchi, hao wanashiriki ufisadi na ulaghai.

Tetesi mojawapo ilionifikia ni kua kiongozi kama Bw Haroun Mwau
alicheza sana hii mipigo lakini hebu tizama yuko wapi sasa?...Jamaa
kakaa kitako Bungeni.Kisha kuna yule Kabogo nadhani alikua mbunge
wa Juja...yeye naye pia nasikia alishiriki/anashiriki haya mambo.
Kuna familia teule hapo Pwani..hususan ile ya kina Akasha...walijulikana
wazi kua wanashughulika maswala ya mihadarati lakini wapi!!!!...
ndume za Central na pale Urban walikua wanakula nao.
Yaani list ni ndefu hata sio siri tena.

Jiulize swali, je iwapo vibosile wetu wanacheza huu mchezo, basi nani
atawazuia walalahoi kutoshiriki?Polisi wenyewe hawatoshi kwa kukwepua
hongo...mnadhani shughuli yenyewe itakoma?...La hasha!

Suluhisho ni nini basi?

Hapa nadhani ni kwa kila aliye na akili timamu asogee mbali na haya madude.
Sidhani kama mtu analazimishwa kutumia bali ni hiari yako mwenyewe na
madhara unayajua.Either utachizika ama utalemaa for life or worse still
utabughudad naswi tutakuzika tu.Ole wako!!!

Tumejaribu kulia na serikali lakini wapi!!!...Huko kumejaa wezi na wabinafsi
chungu tele na tusitarajie msaada wowote wa maana.Vyama vya jamii,
vinaweza kusaidia katika kuelimisha raia kuhusu madhara ya mihadarati but
beyond that sioni kama la maana linaweza kufanywa.

Shukran wakuu.
Hio ni senti yangu hamsini naibwaga sebuleni.
Reply With Quote
  #23 (permalink)  
Old 5th July 2008, 05:27 AM
Senior Member
 
Join Date: Jun 2008
Posts: 232   (View Stats)
BABA KANUSH is on a distinguished road
Not Ranked  0 score     
Default

JayR na wenzako tumieni minyambuliko ya vitenzi na vidokezo kem kem kwenye mjadala huu.
Reply With Quote
  #24 (permalink)  
Old 5th July 2008, 06:24 AM
Senior Member
 
Join Date: Sep 2007
Location: Here
Posts: 967   (View Stats)
Mishky is on a distinguished road
Not Ranked  0 score     
Default Ole wenu

tunawapa pole yanga wakereketwa wa lugha adimu ya kiswahili. Makinikeni bwana na kurasa zenu katika somo hili ili msije mkatuabisha sisi yanga asili.
__________________
Mume ni Madeni
Reply With Quote
  #25 (permalink)  
Old 5th July 2008, 06:40 AM
Senior Member
 
Join Date: Oct 2007
Posts: 1,212   (View Stats)
Titchaz is on a distinguished road
Not Ranked  0 score     
Default

Quote:
Originally Posted by Mishky View Post
tunawapa pole yanga wakereketwa wa lugha adimu ya kiswahili. Makinikeni bwana na kurasa zenu katika somo hili ili msije mkatuabisha sisi yanga asili.
Mishky,

Kamata tano ya nguvu babuu!!!
Nimependa sana wasia wako ulowapa hawa maponjoro wasojua Kiswahili!
Reply With Quote
  #26 (permalink)  
Old 5th July 2008, 06:41 AM
Senior Member
 
Join Date: Oct 2001
Location: .
Posts: 5,868   (View Stats)
KEMINOKANA is an unknown quantity at this point
Not Ranked  0 score     
Default

Now please tell me people like Jay-R had to write Inshas in competition with someone from Lodwar. How unfair?. On top of that, one can tell the difference between a coastarian native and an upcountryman's swahili regardless of the number of vocabularies the latter throws in. LOl waaaa! I'll just sit back and admire.
__________________
Knowledge by hand and mind
Reply With Quote
  #27 (permalink)  
Old 5th July 2008, 06:47 AM
Senior Member
 
Join Date: Sep 2007
Location: Here
Posts: 967   (View Stats)
Mishky is on a distinguished road
Not Ranked  0 score     
Default

Quote:
Originally Posted by Titchaz View Post
Mishky,

Kamata tano ya nguvu babuu!!!
Nimependa sana wasia wako ulowapa hawa maponjoro wasojua Kiswahili!
@ titchaz...
Eeh bwana wee..! wasije wakaopotosha jamaa na wao wenye wakijui wala wanakiigiza tu. Si lugha ya mitaani hii. Ni cha wasom
i kiswahili.
__________________
Mume ni Madeni
Reply With Quote
  #28 (permalink)  
Old 5th July 2008, 12:45 PM
Senior Member
 
Join Date: Oct 2007
Posts: 168   (View Stats)
toobig is on a distinguished road
Not Ranked  0 score     
Default

Quote:
Originally Posted by Jay-R View Post
Swala hili limesikitisha moyo wangu si haba nami sinabudi kuuweka wazi..

Kuna vitongoji fulani mwambao (sitaji majina) ambako wana wa rika fulani watokomea na hata kukata kamba ati kisa na maana ni mihadarati...kushuhudiiiiiia mwenyewe.

Lakusononesha ni kuwa haigharimu hela nyingi pasi na kuwa yapatikana kwa urahisi ,ashuu tu! watia kifurushi mkobani..

Isitoshe, kuna wale wana wachanga (hasa masikini )wanaotumika kama vibaraka kunadi kwa niaba ya wale walanguzi.. ikawa shule haiend*eki tena.. lahaula !...

Kana kwamba haliwahusu , viongozi walotwikwa jukumu na wenye nchi wamekaa ndeeee waangalia uchumi wa nchi hii na viongozi wa kesho wakizorota....

Siwatoi shukrani, wengine walikuwa kajitolea muhanga sijui lipi lilioenda mrama... Jamani, hakutokei msamaria kuwanusuru hawa wana.?..

Mi naona hili ni janga...laiti kama tungezingatia....hii sirikali yetu,yale mashirika yanayohusika na umma kwa jumla, twafaa kukaza kamba na kukomesha mihadarati....hasa mwambao manake ndio ngome...

Oyee,umaskini na ukosefu wa vibarua ndio chanzo cha mihadarati ,kwa hivyo usiwalaumu sana,,,


Otherwise,,,,umefanya jambo poa kwa kubonga kiswahili sanifu hapa manake wengi wa watu hapa hujifanya wazungu weusi...................

Shame on them all dark arsed niggaz from kenya Afrika who are trying to ape the caucasians,,,
Reply With Quote
  #29 (permalink)  
Old 5th July 2008, 02:25 PM
Senior Member
 
Join Date: Apr 2008
Posts: 198   (View Stats)
Genuwine is on a distinguished road
Not Ranked  0 score     
Default

Quote:
Originally Posted by nyira View Post
Swala la madawa ya kulwevya si haba na kwa kinaga limekita mizizi nchini kenya.sio mwambao tu bali pia miji mikubwa nchini.
.
Naomba fursa kuchangia mada hii. Nakubaliana na wewe unaposema kuwa tabia hii imekita mizizi nchini Kenya na hasa mkoa wa pwani. Lakini, swali langu ni...kwa nini ulanguzi wa mihadarati umekomaa sana mkoa wa pwani?

Kwa mfano...ile familia ya Akasha kwa miaka mingi ilijulikana na serekali kuwa ilikuwa kwa biashara ya kuuza mihandarati. Tunajua pia...familia za mabwenyenye mjini mombasa wanapambana na shida za watoto wao kuingilia madawa ya kulevya. Watoto wa hayati mwanasiasa mkongwe wa mombasa pia wako na shida ya madawa ya kulevya. Ni nani ajasikia juu ya mihadarati huko kilifi na malindi?

Mbona mkoa huu unaongoza kwa visa, visanga na mikasa zinazohusiana na mihadarati?
__________________
Take time to be with yourself. It will help you to be with others.
Reply With Quote
  #30 (permalink)  
Old 5th July 2008, 03:08 PM
Senior Member
 
Join Date: Apr 2007
Location: starbucks, corner-most couch
Posts: 1,356   (View Stats)
mtoto mzuri is on a distinguished road
Not Ranked  0 score     
Default

yaonekana nilijinusura wakati iliyofaa kwani sidhani ningewezana na magwiji wa lugha walio miongoni mwetu. bila shaka kiswahili changu sio cha kuvutia kama vile tumeshuhudia! maneno yangu yametapakaa kwote na ngeli yangu, hata mimi mwenyewe siwezi kana, sio safi. huenda hata wazo langu haieleweki vilivyo. lakini kwa upande mwingine, ninaburudika kusoma lugha sanifu hapa mashada. najifunza mapya kwani penye mafund hapakosi wanafunzi. hongera kwa waloshuhudia mjadala huu. msiwache... endeleeni!
Reply With Quote
Reply

Tags
changieni, hapa, hebu, mpo, nina, nyeti, swala, waswahili, wenzangu

Thread Tools
Display Modes

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are On
Pingbacks are On
Refbacks are On



All times are GMT -4. The time now is 08:51 PM.


SEO by vBSEO 3.3.0