Go Back   Mashada Forums » Travel & Places » Around Tanzania
Connect with Facebook

Notices

Reply
 
LinkBack Thread Tools Display Modes
  #1 (permalink)  
Old 3rd August 2009, 03:46 AM
Member
 
Join Date: Jul 2009
Posts: 77   (View Stats)
Tallrays is on a distinguished road
Not Ranked  0 score     
Default Starehe Gharama    Show Printable Version  Print   Email this Page  Email  

Siku hiyo niliwahi kutoka skuli. Tumbo liliniletea `matataizo,’ hali ambayo ilihatarisha hali ya upendo, umoja na mshikamano uliojengwa kwa karne nyingi kule tumboni. Sikuwa na jinsi zaidi ya kujitoma kwenye daladala kuwahi nyumbani. Si wajua vile maskuli yetu hayana kasma ya kumtibisha mwanafunzi?

Kufika tu kituoni, daladala hilo! tena tupu, “limepigwa mswaki” na menziye yaliyozidi kete. Ile naingia tu, konda akanidaka.

“We wa-kusoma! Unakaa kwenye kiti kwani utalipa nauli ya mtu mzima?” Akanizuia kuketi, japo gari liliondoka likiwa bado vile vile `swaki.’

Baada ya kusimama kwa muda, nilihisi hali kuzidi kuwa mbaya, na “breki” niliyodhibitia vilivyomo tumboni ilikaribia kufeli. Na kufeli kwa breki hiyo kungefanya vilivyomo tumboni vitoke kwa kasi isiyo na kidhibiti-mwendo. Na kwa kuwa nilikuwa nimesimama peke yangu kwenye gari tupu, nilionekana na kila abiria. Hivyo basi kitendo cha kufanya `majambozz’ mle mle ndani ya gari kungenigeuza kideo cha bure!

HADITHI KAMILI: Starehe Gharama | East Africa in Focus
Reply With Quote
Reply

Tags
gharama, starehe

Thread Tools
Display Modes

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are On
Pingbacks are On
Refbacks are On



All times are GMT -4. The time now is 12:08 PM.


SEO by vBSEO 3.3.0